Friday, 30 May 2014

BALOTELLI AWABEZA WAINGEREZA KOMBE LA DUNIA BRAZIL

Mshambuliaji wa timu ya taifa  ya Italia Mario Ballotelli amekibeza kikosi cha kocha Roy Hudgson kuwa hakiogopeki kombe ladunia mwaka huu na pia hategemei kuwa wapinzani wakubwa na washindani kwenye michuano hiyo.

akihojiwa na gazeti la Daily Mail baloteli alisema afikilii kama timu ya taifa ya Uingereza kuwa mpinzani mkubwa na mshindi wa kombe la Dunia mwaka huu licha ya kuwa na wachezaji wazuri.

"Sifikilii Uingereza kuwa washindi wa kombe la Dunia mwaka huu licha ya kuwa na wachezaji wazuri lakini si washindani wa Italia". Alinukuliwa Balotelli.

aliendelea kusema kuwa hamaanishi kuwa Italia ni Timu bora katika kombe hili la Dunia bali wanawachezaji wenye morali ya kucheza na kuishangaza Dunia kuliko kikosi cha waingereza. alendelea kubeza kuwa wanawachezaji ambao walishashinda kombe la Dunia wakati waingereza hawana.

Uingereza watacheza na Italia mechi yao ya kwanza tarehe 14 Juni kabla hawajacheza na Uruguay na Kosta rika katika michezo itakayofuatia ya kundi D. Waingereza wacheza na Italia akikumbuka kuondoshwa na hao Waitaliano katika michuano ya EURO 2012 kwa mikwaju ya penati baada ya kudroo 0-0 kwenye hatua ya makundi.

 Balotelli alimaliza kwa kusema Waingereza wanawachezaji wawili au watatu wakuogopwa kwenye kombe la Dunia lakini sio kikosi kizima cha Uingereza. wanajiamini na wana uhakika wa kushinda michezo yao.
source sky sport

No comments:

Post a Comment