michezoni
Wednesday, 19 November 2014
Sunday, 27 July 2014
LIVERPOOL YAMSAJILI DEJAN LOVREN KUTOKA SOUTHAMPTON
Klabu ya soka ya liverpool imekamilisha usajili wa beki wa kati kutoka Southampton Dejan Lovren.
Lovren amehamia liverpool kwa ada ya uhamisho kiasi cha paundi 20 millioni na kuwa beki wakwanza kikosini hapo kusajiliwa kwa gharama kubwa.
Beki huyo ametoa rekodi ndogo iliyowekwa na Mamadou Sakho beki aliyesajiliwa kwa paundi 18 millioni na sasa lovren ndo beki ghali katika historia ya Liverpool.
Uhamisho huu umekamilisha idadi ya wachezaji watatu msimu huu waliohama Southampton na kutimkia Liverpool akijiunga na wenzie Adam Lallana na Rickie Lambert.
Kwa upande wake Lovren amesema ni furaha kujiunga na klabu kubwa katika historia ya soka Uingereza na ndoto yake imetimia ya kucheza chini ya mashabiki wenye hali na moli wa kushangilia.
Brenden Rogers amesema usajili huu ni kuimarisha safu yake ya ulinzi msimu huu lakni pia ni mchezaji mwenye malengo na uongozi mzuri kwa wenzie awapo uwanjani.
source: LFCTV
Tuesday, 22 July 2014
BRAZIL IMEMTEUA DUNGA KUWA KOCHA MPYA WA TIMU YA TAIFA
Brazil imempa kibarua Dunga cha kukinoa kikosi cha timu ya taifa kuziba nafasi ya kocha Scorali aliyejuzulu.
Dunga mwenye umri wa miaka 50 aliweza kuiongoza Brazil kuchukua kombe la Dunia mnamo mwaka 1994 akiwa kama timu kapteni.
Alikinoa kikosi hicho kwenye mashindano ya kombe la Dunia mwaka 2010 huko nchini Afrika ya Kusini na akatimuliwa kibarua hicho baada ya kuondolewa katika mashindano hayo na timu ya taifa ya Uholanzi kwenye hatua ya robo fainali.
Scorali pia alijiuzulu kukinoa kikoso hicho baada ya kuondolewa kama mwenyeji kwenye mashindano ya kombe la Dunia kama mwenyeji kwa kufungwa goli 7-1 na Ujerumani mabingwa wa mwaka huu.
Dunga kapewa kikosi hicho kwa imani kubwa ya kuleta mabadiliko na kuizoea timu mapema kwa muda mrefu iliwaweze kuja fanya mabadiliko baadae.
MADRID IMEKAMILISHA UHAMIMISHO WA MCHEZAJI JAMES RODRIGUEZ
Klabu ya soka ya Mdrid imefanikisha kumsajili mchezaji wa timu ya taifa ya Colombia na klabu ya Monaco James Rodriguez.
Madrid imekamilisha uhamisho wa Rodriguez kwa ada ya paundi milioni 68 kutoka klabu yake ya Monaco aliyo iwezesha kucheza UEFA.
Nyota huyo wa Colombia aliweza kung'aa zaidi katika mashindano ya kombe la Dunia yaliyo malizika huko nchini Brazil wiki chache zilizopita.
Rodriguez mwenye umri wa miaka 23 sasa atajiunga na mastaa wa soka wa klabu ya Madrid yaani Ronaldo, Bale, Benzema na wengine wengi.
Klabu yake ya Monaco imetoa shukurani za dhati kwa mchezaji huyo aliyeweza kufunga magoli tisa na kutoa pasi za magori 12.
Amesaini mkataba wa miaka sita ndani ya klabu ya Madrid ya huko Uhispania.
Monday, 21 July 2014
STEVEN GERALD ATANGAZA KUSTAAFU
Kapteni wa timu ya taifa ya Uingereza Steven Gerald ametangaza kustaafu kuichezea timu ya taifa.
Steven Gerald amefikia uamuzi huo baada ya haya mashindano ya kombe la Dunia huko nchini Brazil kupita.
Ametoa shukrani za dhati kwa mashabiki wa timu ya taifa na makocha wote aliofanya nao kazi chini ya timu ya taifa.
Gerald amesema sasa anaelekeza juhudi zote kwenye klabu yake ya Liverpool ambayo sasa imefuzu tayari mashindano ya UEFA.
Hakusita kumshukuru kocha Roy Hudgson ambaye alimpa mamlaka ya ukapteni wa timu ya taifa tangu apewe timu hiyo nakusema ameifanya ndoto yake ya utotoni kutimia.
Gerald amemalizia kwa kisema kustaafu kwake majukumu ya timu taifa haimanishi anaitelekeza timu hiyo bali tabaki kufaya kazi na shirikisho la soka nchini humo yaani FA.
ROONEY APANAIA KUMSHANGAZA KOCHA WAKE VAN GAL
Mchezaji wa klabu ya soka ya Manchester United Wayne Rooney amesema yupo tayari kumshangaza kocha wake mpya Van gal baada ya kuanza kufanya nae mazoezi.
Rooney amesema yupo tayari kufanya kila awezalo mazoezini ili kumuonesha uwezo wake kocha huyo mpya kutoka nchini Uholanzi.
Van gal anatarajiwa kutangaza kapteni wake klabuni hapo wakati wowote ambapo macho mengi yakiwa ni kwa Van persie ama Rooney.
Van persie amekua kepteni wa timu ya taifa chini ya kocha huyo huyo mholanzi ambaye amekifikisha kikosi nafasi ya tatu katika mashindano yaliyokamilika ya kombe la Dunia huko nchini Brazil.
Rooney pia anapewa nafasi kubwa kutokana na ukweli kuwa amekuwa na ushawishi mkubwa ndani ya klabu hiyo na nikiongozi mzuri wa wachezaji wenzake.
Rooney amesema huu ndo wakati wa kumuonesha kocha kile walichonacho wachezaji ili kumrahisishia upangaji wa kikosi cha Man U.
Wachezaji wengine pia kama Mata wanasema wamejiandaa vizuri kutetea klabu ya licha ya kuwa na matokeo magumu katika timu ya taifa iliyoondolewa mapema kwenye mashindano ya kombe la Dunia huko Brazil.
ISCO WENDA AKAHAMIA LIVERPOOL
Mshambuliaji wa kilabu la Real Madrid ya Uhisipania Isco wenda akahamia nchini Uingereza kwenye klabu ya soka ya Liverpool
Taarifa za awali zinasema kuwa liverpool wanajipanga kutuma ofa ya kumsajili mshambuliaji huyo ili kuziba mwanya ulioachwa na mshambuliaji Luis Suarez ailyesajiliwa Barcelona.
Liverpool wametenga kiasi cha paundi milioni 80 kuweza kusajili wachezaji wanao fikiliwa kuwa mbadala wa Suarez.
Kwa upande wake Isco wenda akavutiwa na ofa hii kutokana na ukweli kwamba yeye ndiye atakua mshambuliaji wa mwisho tofauti na Real Madrid anakocheza nyuma ya Mshambuliaji.
Isco ameweza kucheza mechi kadhaa chini ya kikosi cha kocha Carlo Ancheloti licha ya kuwa hana namba ya kudumu kwenye kikosi hicho.
Liverpool wamekuwa wakiaswa kutorudia makosa yaliyo igharimu klabu ya Tottenham baada ya kumuuza Gareth Bale na kukosa mbadala wake yasije tokea pia kwa Liverpool kwa kumuuza Suarez.