Tuesday, 22 July 2014

BRAZIL IMEMTEUA DUNGA KUWA KOCHA MPYA WA TIMU YA TAIFA

Brazil imempa kibarua Dunga cha kukinoa kikosi cha timu ya taifa kuziba nafasi ya kocha Scorali aliyejuzulu.

Dunga mwenye umri wa miaka 50 aliweza kuiongoza Brazil kuchukua kombe la Dunia mnamo mwaka 1994 akiwa kama timu kapteni.

Alikinoa kikosi hicho kwenye mashindano ya kombe la Dunia mwaka 2010 huko nchini Afrika ya Kusini na akatimuliwa kibarua hicho baada ya kuondolewa katika mashindano hayo na timu ya taifa ya Uholanzi kwenye hatua ya robo fainali.

Scorali pia alijiuzulu kukinoa kikoso hicho baada ya kuondolewa kama mwenyeji kwenye mashindano ya kombe la Dunia kama mwenyeji kwa kufungwa goli 7-1 na Ujerumani mabingwa wa mwaka huu.

Dunga kapewa kikosi hicho kwa imani kubwa ya kuleta mabadiliko na kuizoea timu mapema kwa muda mrefu iliwaweze kuja fanya mabadiliko baadae.

No comments:

Post a Comment