Klabu ya soka ya liverpool imekamilisha usajili wa beki wa kati kutoka Southampton Dejan Lovren.
Lovren amehamia liverpool kwa ada ya uhamisho kiasi cha paundi 20 millioni na kuwa beki wakwanza kikosini hapo kusajiliwa kwa gharama kubwa.
Beki huyo ametoa rekodi ndogo iliyowekwa na Mamadou Sakho beki aliyesajiliwa kwa paundi 18 millioni na sasa lovren ndo beki ghali katika historia ya Liverpool.
Uhamisho huu umekamilisha idadi ya wachezaji watatu msimu huu waliohama Southampton na kutimkia Liverpool akijiunga na wenzie Adam Lallana na Rickie Lambert.
Kwa upande wake Lovren amesema ni furaha kujiunga na klabu kubwa katika historia ya soka Uingereza na ndoto yake imetimia ya kucheza chini ya mashabiki wenye hali na moli wa kushangilia.
Brenden Rogers amesema usajili huu ni kuimarisha safu yake ya ulinzi msimu huu lakni pia ni mchezaji mwenye malengo na uongozi mzuri kwa wenzie awapo uwanjani.
source: LFCTV
No comments:
Post a Comment