Tuesday, 22 July 2014

MADRID IMEKAMILISHA UHAMIMISHO WA MCHEZAJI JAMES RODRIGUEZ

Klabu ya soka ya Mdrid imefanikisha kumsajili mchezaji wa timu ya taifa ya Colombia na klabu ya Monaco James Rodriguez.

Madrid imekamilisha uhamisho wa Rodriguez kwa ada ya paundi milioni 68 kutoka klabu yake ya Monaco  aliyo iwezesha kucheza UEFA.

Nyota huyo wa Colombia aliweza kung'aa zaidi katika mashindano ya kombe la Dunia yaliyo malizika huko nchini Brazil wiki chache zilizopita.

Rodriguez mwenye umri wa miaka 23 sasa atajiunga na mastaa wa soka wa klabu ya Madrid yaani Ronaldo, Bale, Benzema na wengine wengi.

Klabu yake ya Monaco imetoa shukurani za dhati kwa mchezaji huyo aliyeweza kufunga magoli tisa na kutoa pasi za magori 12.

Amesaini mkataba wa miaka sita ndani ya klabu ya Madrid ya huko Uhispania.

No comments:

Post a Comment