Mshambuliaji wa kilabu la Real Madrid ya Uhisipania Isco wenda akahamia nchini Uingereza kwenye klabu ya soka ya Liverpool
Taarifa za awali zinasema kuwa liverpool wanajipanga kutuma ofa ya kumsajili mshambuliaji huyo ili kuziba mwanya ulioachwa na mshambuliaji Luis Suarez ailyesajiliwa Barcelona.
Liverpool wametenga kiasi cha paundi milioni 80 kuweza kusajili wachezaji wanao fikiliwa kuwa mbadala wa Suarez.
Kwa upande wake Isco wenda akavutiwa na ofa hii kutokana na ukweli kwamba yeye ndiye atakua mshambuliaji wa mwisho tofauti na Real Madrid anakocheza nyuma ya Mshambuliaji.
Isco ameweza kucheza mechi kadhaa chini ya kikosi cha kocha Carlo Ancheloti licha ya kuwa hana namba ya kudumu kwenye kikosi hicho.
Liverpool wamekuwa wakiaswa kutorudia makosa yaliyo igharimu klabu ya Tottenham baada ya kumuuza Gareth Bale na kukosa mbadala wake yasije tokea pia kwa Liverpool kwa kumuuza Suarez.
No comments:
Post a Comment