Kapteni wa timu ya taifa ya Uingereza Steven Gerald ametangaza kustaafu kuichezea timu ya taifa.
Steven Gerald amefikia uamuzi huo baada ya haya mashindano ya kombe la Dunia huko nchini Brazil kupita.
Ametoa shukrani za dhati kwa mashabiki wa timu ya taifa na makocha wote aliofanya nao kazi chini ya timu ya taifa.
Gerald amesema sasa anaelekeza juhudi zote kwenye klabu yake ya Liverpool ambayo sasa imefuzu tayari mashindano ya UEFA.
Hakusita kumshukuru kocha Roy Hudgson ambaye alimpa mamlaka ya ukapteni wa timu ya taifa tangu apewe timu hiyo nakusema ameifanya ndoto yake ya utotoni kutimia.
Gerald amemalizia kwa kisema kustaafu kwake majukumu ya timu taifa haimanishi anaitelekeza timu hiyo bali tabaki kufaya kazi na shirikisho la soka nchini humo yaani FA.
No comments:
Post a Comment