Beki wa Arsenal na timu ya taifa ya Ufaransa Bacary Sagna ametangaza rasmi kuiacha klabu hiyo ya jijini London nchini Uingereza.
akizungumza na gazeti la French newspaper L’Equipe la nchini kwao alisema amefikia uamuzi wa kuiacha klabu ya Arsenal aliyoichezea kwa takribani miaka 10 baada ya kutofikia muafaka wa mazungumzo kati yake na klabu.
Vilabu kama Liverpool na Man city vimekua vikimuhitaji beki huyo na Man city wao wakifikia mbali kwa kumuaidi donge nono endapo atjiunga nao msimu ujao wa ligi kuu ya nchini Uingereza.
"Sio siri tena kwa sasa ntaondoka Arsenal, nimejaribu niwezavyo lakini sijafanikiwa kutokana na mazungumzo baina yangu mimi na klabu kutoenda sawa, napokea simu nyingi nikihitajika timu kadha wa kadha mpaka zinaniumisha kichwa, lakini nategemea kufikia muafaka kabla ya kwenda kombe la Dunia". Alisema Sagna
Kwa upande wao Arsenal watamkosa kwa kiasi kikubwa beki huyo kwani kwa kipindi chote alichokuepo klabuni hapo amekua ni msaada mkubwa kwa klabu hiyo ya jijini London.

No comments:
Post a Comment