Goli kipa wa klabu ya Manchester United Mhisipania David Degea amesema ameanza kumshauri Mhisipania mwenzie Cesc Fabregas kujiunga nae katika klabu ya Man u ya nchini Uingereza.
Fabregas ambaye ni mchezaji wa klabu ya Barcelona kumekua na taarifa kuwa anahitaji kuhama badada ya msimu huu uliomalizika.
"Nimekua nikimshawishi Fabregas kujiunga na Man u". alisikika akisema Goli kipa huyo wa Man u alipokua kwenye mahojiano na kituo kimoja cha luninga nchini Hispania.
Degea anakutana na wakati kumgumu kumshauri Fabregas kuiacha klabu yake ya Hispania FC BARCELONA kujiunga na klabu yake ya Man u kwani msimu uliopita aliyekua kocha wa Man u David Moyes Tayari alishashindwa.
Kocha wazamani wa Fabrigas ambaye ndiye kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amekua akimhitaji kumrudisha kikosini, hivyo ni upinzani mkubwa watakao kutana nao Man u kumshawishi kujiunga nao chini ya kocha wao mpya Van Gaal.
Ushawishi wa Degea unawapa nafasi kubwa Man u kumtwaa Febregas kutokana na ukweli kuwa klabu ya Arsenal inao viungo wa katikati tayari, kama Ozil, Wilshire na Cazorla, ambao wataleta swali gumu la wapi au nafasi gani Fabregas atacheza?

No comments:
Post a Comment