Sunday, 1 June 2014

LIVERPOOL WAONGEZA DAU KUMSAJILI LALLANA

Klabu ya soka ya Liverpool ya nchini Uingereza iliyopo mbioni kumsajili kiungo wa Southampton Adam Lallana imeongeza dau kiasi cha paundi milioni 5 ilikunasa saini ya mchezaji huyo baada ya dau la awali kukataliwa.

Mwanzoni Liverpool walitenga kiasi cha paundi milioni 20 ambazo zilikataliwa na klabu ya Southampton kama dau la kumwachia kiungo wao. Tayari Liverpool washafikia makubaliano ya kumchukua beki mwingine wa klabu hiyo Rickie Lambert ambaye tayari keshafanyiwa na vipimo vya kiafya.

Licha ya Liverpool kutangaza dau hilo bado Southampton wanaoneka kusimamia msimamo wao wa paundi milioni 30 ndo wamwachie kiungo huyo aliyekua moja ya chachu ya timu kumaliza nafasi ya nane kwenye msimamo wa ligi msimu uliomalizika.

kocha Brenden Rogers anaonesha wazi wazi kumhitaji kiungo huyo ili kuimarisha timu yake ya msimu ajao akipewa sapoti na baadhi ya viongozi wa timu, bila shaka inaonesha watafikia muafaka kabla ya kombe la Dunia kukamilika.

No comments:

Post a Comment