Liverpool mbioni kumnasa kiungo wa Southampton Adam Lallana baada ya klbu ya Tottenham kujitoa kwenye kinyang'anyiro cha kumsaka.
Awali ilisemekana lallana angejiunga na Tottenham kumfuata kocha wake aliyekuwa akimfundisha Southampton aliyepata kibarua hicho siku si nyingi klabuni hapo.
Liverpool tayari walishaongeza dau la kiasi cha paundi millioni 25 kutoka ile ya awali paundi millioni 20 lakini Southampton wanaonesha kusimamia msimamo wao ule ule wakuitaji paundi millioni 30.
Kwa upande wake mchezaji Adam Lallana anonesha kuzidi kuvutiwa zaidi na Liverpool mara baada ya mchezaji mwenzie walie kuwa nae southampton kujiunga na Liverpool yaani Rickie Lambert, hii imezidi kumvuta zaidi Lallana ndaani ya Anfield .
Lallana ni mchezaji mwenye uwezo mkubwa anapo cheza katikati kama kiungo mshambuliaji na anaonekana kuwa msaada mkubwa kwa liverpool pale atakapo kuwa nyuma ya washambuliaji hatari wa Liverpool yaani Suarez na Sturridge.


No comments:
Post a Comment