Monday, 9 June 2014

HATIMA YA WAMBURA NDANI YA UCHAGUZI WA SIMBA KUJULIKANA LEO

Hatima ya Wambura kugombea uraisi ndani ya klabu ya simba kujulikana leo baada ya tume ya rufaa ya TFF kukutana leo kujadili rufaa yake aliyoipeleka mahakamani kupinga kuzuiwa kugombea uraisi ndani ya klabu ya simba.

kamati ya uchaguzi ya simba chini ya mwenyekiti wake Damas Ndumbaro walifikia uamuzi wa kumsimamisha Michael Wambura kama mgombea wa uraisi wakidai kuwa haukuwa na uanachama hai ndani ya klabu.

Baada ya wambura kusimamishwa alifikia uamuzi wa kukata rufaa ndani ya kamati ya rufaa ya TFF kupinga uamuzi wa kusimamishwa kugombea uongozi ndani ya klabu ya simba.

Wambura alisema amekua mwanachama hai wa klabu ya simba tena aliye hai na alishiriki kuiweka madarakani tume hiyo ya uchaguzi iliyomsimamisha kugombea uraisi wa TFF, wakati upande wao tume kuendelea kudai kutomjua Wambura kama mwanachama hai ndani ya klabu.

No comments:

Post a Comment