Baba wa mchezaji wa Man City Yahaya Toure amethibitisha kuwa mwanae ataendela kubaki ndani ya klabu hiyo kutokamna na uvumi uliojitokeza kwamba angeondoka klabuni hapo kutokana na kutothaminiwa licha ya uwezo alioonesha klabini hapo.
Klabu ya Ufaransa ya PSG walionesha nia mamepema nia ya kumhitaji mchezaji huyo ambaye kwa sasa ameonekana kuwa na uwezo mkubwa baada ya kuisaidia klabu yake kubeba ubingwa wa soka nchini Uingereza.
Yahaya Tuoure alitegemewa kuondoka klabuni hapo kutokana na maneno yaliyokuwa yakitolewa na wakala wake kwamba angeondoka kutokana na kutothaminiwa na uongozi wa juu wa klabu hiyo ya Man City.
Baba mzazi huyo aliendelea kusema mwanae ni mtu ambaye huwa hafurahi kuwa kwenye mazingira magumu kwake au yasiyo mpendeza, alisema anamini hayo yatamalizika na mwanae ataendelea kufurahia maisha yake ndani ya ETIHAD.

No comments:
Post a Comment