Huyu ndiye Ronadihno feki aliyevamia mazoezi ya timu ya taifa ya Argentina ili kumuona Lionel Messi, shabiki huyo anae fanana kupitiliza na Ronadihno alitokea kusiko julikana na kuwaadaa walinzi kama Ronadinho kwa kuingia uwanjani kwa mbio kumfuata Messi.
Alipomfikia Messi alibidi Messi ashangae na kumuuliza Ronadinho feki kwa nini amefikia uamuzi huo kwa sababu akiitaji kuonana nae hana haja ya kufanya hivyo, alipofika kwa Messi na kumpa mkono, alimshangaza zaidi pale alipo mpigia magoti.
Alopotolewa na wanausalama na kuhojiwa alisema hakuwa na jinsi nyingine ya kumuona messi na kumuonesha jinsi gani anamkubali zaidi ya hiyo ya kutumia nafasi ya ufanano wake na Ronadihno kutimiza ndoto zake.
Kwa upande wake mwssi alibaki kuduwaa na kumshangaa mtu huyo mwisho wake aliishia kumfurahia, Argentina ndio timu inayopata washabiki wengi mazoezini wanaotazama uwezo wa wachezaji hao.
Alipoulizwa ni mchezaji gani mwingine anampenda kiasi hicho ni nani hakusita kumtaja pacha wake wa bandia yaani Ronadinho.

No comments:
Post a Comment