Thursday, 12 June 2014

KITAZAME KIKOSI CHA BRAZIL KINACHOANZA LEO DHIDI YA CROATIA

Leo ndo leo ufunguzi wa kombe la Dunia ndani ya nchi ya Brazil ambapo tutawashudia wenyeji Brazil wawaalika Croatia kufungua rasmi michuano hiyo. Mechi hiyo inakadiliwa kuchezwa mishale ya saa 5 usiku kwa saa za Afrika Mashariki

MTAZAME RONADIHNO FEKI ALIYEVAMIA MAZOEZI YA ARGENTINA ILI KUMUONA MESSI

Huyu ndiye Ronadihno feki aliyevamia mazoezi ya timu ya taifa ya Argentina ili kumuona Lionel Messi, shabiki huyo anae fanana kupitiliza na Ronadihno alitokea kusiko julikana na kuwaadaa walinzi kama Ronadinho kwa kuingia uwanjani kwa mbio kumfuata Messi.

Alipomfikia Messi alibidi Messi ashangae na kumuuliza Ronadinho feki kwa nini amefikia uamuzi huo kwa sababu akiitaji kuonana nae hana haja ya kufanya hivyo, alipofika kwa Messi na kumpa mkono, alimshangaza zaidi pale alipo mpigia magoti.

Alopotolewa na wanausalama na kuhojiwa alisema hakuwa na jinsi nyingine ya kumuona messi na kumuonesha jinsi gani anamkubali zaidi ya hiyo ya kutumia nafasi ya ufanano wake na Ronadihno kutimiza ndoto zake.

Kwa upande wake mwssi alibaki kuduwaa na kumshangaa mtu huyo mwisho wake aliishia kumfurahia, Argentina ndio timu inayopata washabiki wengi mazoezini wanaotazama uwezo wa wachezaji hao.

Alipoulizwa ni mchezaji gani mwingine anampenda kiasi hicho ni nani hakusita kumtaja pacha wake wa bandia yaani Ronadinho.

Wednesday, 11 June 2014

BABA WA YAHAYA TOURE ATHIBITISHA MWANAE KUENDELEA KUWEPO MAN CITTY

Baba wa mchezaji wa Man City Yahaya Toure amethibitisha kuwa mwanae ataendela kubaki ndani ya klabu hiyo kutokamna na uvumi uliojitokeza kwamba angeondoka klabuni hapo kutokana na kutothaminiwa licha ya uwezo alioonesha klabini hapo.

Klabu ya Ufaransa ya PSG walionesha nia mamepema nia ya kumhitaji mchezaji huyo ambaye kwa sasa ameonekana kuwa na uwezo mkubwa baada ya kuisaidia klabu yake kubeba ubingwa wa soka nchini Uingereza.

Yahaya Tuoure alitegemewa kuondoka klabuni hapo kutokana na maneno yaliyokuwa yakitolewa na wakala wake kwamba angeondoka kutokana na kutothaminiwa na uongozi wa juu wa klabu hiyo ya Man City.

Baba mzazi huyo aliendelea kusema mwanae ni mtu ambaye huwa hafurahi kuwa kwenye mazingira magumu kwake au yasiyo mpendeza, alisema anamini hayo yatamalizika na mwanae ataendelea kufurahia maisha yake ndani ya ETIHAD.

HAKUNA MIUJIZA KATIKA MAFANIKIO YA SOKA - MWENYEKITI MBEYA CITY

Mwenyekiti wa klabu ya soka ya Mbeya City Bw Musa Mapunda amesma hakuna miujiza siku zote katika mchezo wa mpira wa miguu. aliyasema hayo kufuatia mafanikio makubwa waliyoyapata klabu ya Mbeya City kwenye ligi ya Tanzania Bara mwaka 2013/2014, licha ya kutobeba ubingwa.

Mbeya City ni klabu iliyopanda daraja msimu uliopita nakufanikiwa kumaliza katika nafasi ya tatu ya ligu kuu ya Tanzania bara, na kuzipiku timu kubwa kama Simba, Kagera sugar na Mtibwa.

Alisema Mpira wa miguu hauna miujiza zaidi ya uongozi mzuri na wenye malengo ya mafanikio ndani ya klabu na kubeza timu kubwa kuwa migogoro wliyonayo ndani ya vilabu vyao ndo chanzo cha timu timu hizo kubwa kuvurunda kisoka.

Aliendelea kusema kuwa kinacho tokea hivi sasa ni watu wenye uchu na madaraka kugombea nafasi ndani ya vilabu vyao ili kutimiza malengo yao binafsi bila kujali maslahi ya timu, kitu ambacho ni makosa makubwa kwa mwenendo wa soka la timu na taifa kwa ujumla.

Kwa sasa Mbeya City wamepata uzamini mkubwa toka kampuni ya kuuza matairi ya magari ya Binslum, Ambayo inakadiliwa kuweka kiasi cha shilingi milioni 360 kwenye mkataba wa udhamini kati ya kmpuni hiyo yenye makazi yake jijini Dar es salaam na klabu hiyo ya jijini Mbeya.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Mbeya City aliendelea kusema kuwa soka ni biashara na ili ufanikiwe unahitaji kuwekeza kiasi kikubwa na kusema timu yao inajipanga vizuri kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu ya soka Tanzania bara.

Tuesday, 10 June 2014

VITAZAME BAADHI YAVITUKO MPIRANI VUNJA MBAVU HAPA

YATAZAME BAADHI YA MAGOLI MAZURI YA LUIS SUAREZ YA MWAKA 2014

RONALDO AKILI MESSI KUWA BORA HATA BILA KUBEBA KOMBE LA DUNIA

Mkongwe wa soka nchini Brazil Ronaldo De Lima amekili kuwa mshambuliaji wa Argentina na klabu ya soka ya Barcelona Lionel Messi kuwa bora kama mchezaji wa Dunia hata kama hatapata mafanikio makubwa kwenye kombe la Dunia nchini Brazil.

Mshindi mara nne wa tuzo ya soka ya Dunia (Ballon D'Or) Lionel Messi amekua akipokea sifa kadha wa kadha kutoka kila upande Duniani kwa staili yake ya uchezaji mpira anayewavutia walo wengi, ndani ya umri wake wa miaka 26.

Licha ya kumsifia Ronaldo, alisema kuwa bado ana umri mdogo na anuwezo wa kufanya makubwa zaidi kwenye soka kuliko haya tunayoshuhudia sasa, kwa upande mwingine Ronaldo alipinga Messi kuitwa Mungu wa mpira akisema kuwa bado anahitaji kuonyesha uwezo zaidi ya huu alionaosasa kuitwa hilo jina.

Kwa upande mwingine hakuacha kumtaja wajina wake Mreno Christian Ronaldo nakusema kuwa ni mchezaji mzuri alistaili kuchukua tuzo ya Dunia iliyopita kwani alionyesha uwezo, lakini pia amekuwa akiwafurahisha  wale mashabiki wa Real Madrid kama yeye kwa kuisadia timu kufanya vizuri.

MAN U KUMLIPA LUKE SHAW PAUNDI 160,000 KWA WIKI KAMA MSHARA

Man U wamefikia makubaliano binafsi na mchezaji Luke Shaw wa Southampton kwa kukubaliana kumlipa mshahara wa kiasi cha paundi 160,000 endapo watafanikiwa kupata saini yake kama mchezaji wao.

Beki huyo ambaye atatimiza miaka 19 mwezi ujao wa saba, endapo atajiunga na Man U na kupewa kiasi hicho cha fedha atakuwa ndo mchezaji kinda (mwenye umri mdogo) Duniani kulipwa mshahara mrefu.

kwa hofa hiyo Man U  watakaua wamewapiku Chelsea ambao nao walimwandalia donge nono mchezaji huyo. Morihno alivutiwa na beki huyo wa pembeni akimhitaji kuziba mwnya wa Ashley Cole ambaye anonekana kutokuwa mvuto tena kwake.

United wamekwisha andaa kiasi cha paundi millioni 27 kwa ajili ya Southamton kama dau la kumsajilia mchezaji huyo.

Southampton wanonekan kuwa wagumu kutoa mchezaji wao kwa sasa wakisubiri mpaka aptikane kocha mpya wa kukinoa kikosi hicho kufuatia aliyekuwa kocha wao kupewa kibarua na Tottnham kuziba nafasi ya kocha aliyeondoka.

Monday, 9 June 2014

HATIMA YA WAMBURA NDANI YA UCHAGUZI WA SIMBA KUJULIKANA LEO

Hatima ya Wambura kugombea uraisi ndani ya klabu ya simba kujulikana leo baada ya tume ya rufaa ya TFF kukutana leo kujadili rufaa yake aliyoipeleka mahakamani kupinga kuzuiwa kugombea uraisi ndani ya klabu ya simba.

kamati ya uchaguzi ya simba chini ya mwenyekiti wake Damas Ndumbaro walifikia uamuzi wa kumsimamisha Michael Wambura kama mgombea wa uraisi wakidai kuwa haukuwa na uanachama hai ndani ya klabu.

Baada ya wambura kusimamishwa alifikia uamuzi wa kukata rufaa ndani ya kamati ya rufaa ya TFF kupinga uamuzi wa kusimamishwa kugombea uongozi ndani ya klabu ya simba.

Wambura alisema amekua mwanachama hai wa klabu ya simba tena aliye hai na alishiriki kuiweka madarakani tume hiyo ya uchaguzi iliyomsimamisha kugombea uraisi wa TFF, wakati upande wao tume kuendelea kudai kutomjua Wambura kama mwanachama hai ndani ya klabu.

AC MILLAN WAMTIMUA RASMI KOCHA WAO CLARENCE SEEDORF

Klabu ya soka ya nchini Uitaliano ya Ac milan imemtimua rasmi kocha wake Clarence Seedorf na kumpa kibarua hicho aliyekuwa mchezaji wake wa zamani philipo Inzag ambaye alikuwa akitumika kama kocha wa timu B ya Ac Milan.

Ac Milan wamefikia uamuzi huo baada ya mwenendo wa kocha Seedorf kutokuwa mzuri tangu alipopokea timu kutoka kwa kocha Massimilliano ambaye pia alitimuliwa na klabu hiyo baada ya mwenendo wa timu kuwa mbovu.

habari za kutimuliwa seedorf zimetolewa na klabu ya Ac milan kupitia mtandao wao rasmi ambao  ulithibitisha uteuzi wa kocha Inzaghi kuwa kocha mkuu ambaye amesaini mkataba wa takribani miaka miwili.

Mholanzi Seedorf amekua na mazingira magumu ndani ya klabu hiyo tangu alipopokea toka kwa kocha Massimiliano na kuhisababishia timu kupata matokeo mabovu hadi mwisho wa msimu.

Tuesday, 3 June 2014

TAZAMA VIDEO YA MCHEZA MIELEKA BATISTA AKITANGAZA KUJITOA WWE

Batista alifikia uamuzi huo mara baada ya kunyimwa pambano na The shield. na baadae kuposti kwenye ukurasa wake wa twitter maneno yaliyosomeka i dont need WWE, WWE needs me, akimaanisha sihitaji WWE, WWE inanihitaji.

LIVERPOOL MBIONI KUMNASA ADAM LALLANA

Liverpool mbioni kumnasa kiungo wa Southampton Adam Lallana baada ya klbu ya Tottenham kujitoa kwenye kinyang'anyiro cha kumsaka.

Awali ilisemekana lallana angejiunga na Tottenham kumfuata kocha wake aliyekuwa akimfundisha Southampton aliyepata kibarua hicho siku si nyingi klabuni hapo.

Liverpool tayari walishaongeza dau la kiasi cha paundi millioni 25 kutoka ile ya awali paundi millioni 20 lakini Southampton wanaonesha kusimamia msimamo wao ule ule wakuitaji paundi millioni 30.

Kwa upande wake mchezaji Adam Lallana anonesha kuzidi kuvutiwa zaidi na Liverpool mara baada ya mchezaji mwenzie walie kuwa nae southampton kujiunga na Liverpool yaani Rickie Lambert, hii imezidi kumvuta zaidi Lallana ndaani ya Anfield .



Lallana ni mchezaji mwenye uwezo mkubwa anapo cheza katikati kama kiungo mshambuliaji na anaonekana kuwa msaada mkubwa kwa liverpool pale atakapo kuwa nyuma ya washambuliaji hatari wa Liverpool yaani Suarez na Sturridge.

Sunday, 1 June 2014

VITAZAME BAADHI YA VITUKO VYA KOCHA ARSENE WENGER

https://www.youtube.com/watch?v=2EIMBuORLpc

LIVERPOOL WAONGEZA DAU KUMSAJILI LALLANA

Klabu ya soka ya Liverpool ya nchini Uingereza iliyopo mbioni kumsajili kiungo wa Southampton Adam Lallana imeongeza dau kiasi cha paundi milioni 5 ilikunasa saini ya mchezaji huyo baada ya dau la awali kukataliwa.

Mwanzoni Liverpool walitenga kiasi cha paundi milioni 20 ambazo zilikataliwa na klabu ya Southampton kama dau la kumwachia kiungo wao. Tayari Liverpool washafikia makubaliano ya kumchukua beki mwingine wa klabu hiyo Rickie Lambert ambaye tayari keshafanyiwa na vipimo vya kiafya.

Licha ya Liverpool kutangaza dau hilo bado Southampton wanaoneka kusimamia msimamo wao wa paundi milioni 30 ndo wamwachie kiungo huyo aliyekua moja ya chachu ya timu kumaliza nafasi ya nane kwenye msimamo wa ligi msimu uliomalizika.

kocha Brenden Rogers anaonesha wazi wazi kumhitaji kiungo huyo ili kuimarisha timu yake ya msimu ajao akipewa sapoti na baadhi ya viongozi wa timu, bila shaka inaonesha watafikia muafaka kabla ya kombe la Dunia kukamilika.